Posts

Showing posts from April, 2014

Real Madrid yafuzu kwa fainali

Image
Vigogo wa ligi kuu ya Uhispania Real Madrid, wamekuwa timu ya kwanza kufuzu kwa fainali ya ligi ya mabingwa barani ulaya baada ya kuinyeshea Mabingwa watetezi wa kombe hilo Bayern Munich ya Ujerumani kwa mabao manne kwa nunge na hivyo kuibuka a ushindi mkubwa wa jumla ya mabao 5-0. Sergio Ramos alifunga mabao mawili mapema katika kipindi cha kwanza cha mechi Bao hilo lilikuwa lake la 16 katika ligi ya mabingwa barani Uropa.Kabla ya nyota wa Ureno na mchezaji bora duniani Christiano Ronaldo kuihakikishia Madrid fainali yao ya kwanza tangu mwaka wa 2002 na mkwaju wa wa freekick. Kwa Bayern, kichapo hicho kilikuwa ni kama wembe wa kutu kwao kwani mwaka uliopita Wajerumani hao waliifunga Barcelona 7-0 katika hatua ya nusu fainali kabla ya kuilaza Borussia Dortmund na kutwaa taji lao la tano barani ulaya. Haijulikani kufikia sasa iwapo halmashauri inayoingoza klabu hiyo itachukua hatua yeyote dhidi ya kocha wa klabu hicho Pep Guardiola ambaye licha ya kuiongoza Barca kutwaa taji la Bu...

Ronaldo avunja rekodi ya Messi

Image
Nyota wa Real Madrid ya Uhispania Cristiano Ronaldo amevunja rekodi ya Lionel Messi ya ufungaji mabao mengi zaidi katika ligi ya mabingwa barani Uropa alipoifungia timu yake mabao mawili na kuisaidia kuichapa Bayern Munich mabao 4-0 katika nusu fainali jana usiku. Kufuatia ushindi huo Real Madrid ilifuzu kwa fainali ya mchuano huo kwa jumla ya mabao 5-0.Mreno huyo mwenye umri wa miaka , 29,alifunga bao lake la 15 na 16 msimu huu katika uwanja wa Allianz Arena. Ronaldo sasa amefunga mabao 16 katika mechi kumi za ligi hiyo ya mabingwa Barani Ulaya mbili zaidi ya Lionel Messi wa Barcelona . Rekodi hiyo ya mabao 14 ilikuwa ikishikiliwa kwa pamoja kati ya Messi (2011-12, Barcelona), Ruud van Nistelrooy (2002-03, Manchester United) na Jose Altafini (1962-63, AC Milan). Kwa jumla Ronaldo amefunga mabao 67 katika ligi hiyo ya mabingwa barani ulaya sawa na Messi na ni mabao manne tu nyuma ya rekodi ya idadio kubwa zaidi ya mabao yaliyofungwa na mchezaji wa zamani wa Real na Schalke Ra...

Rais wa Brazil amuunga mkono Alves

Image
Rais wa Brazil amuunga mkono Alves kwa kula ndizi Rais Dilma Rousseff, amesifu kitendo cha mchezaji wa kimataifa wa Brazil, na Barcelona Dani Alves kutokana na tukio la ubaguzi wa rangi wakati wa mechi ya ligi kuu ya Uhispania, La Liga kati ya Barcelona na Villareal . Bi Rousseff aliandika katika mtandao wake wa twitter kuwa Dani Alves alionyesha ujasiri wa kukabiliana na ubaguzi wa rangi katika kandanda na kuwa ni tukio la kuigwa .Mchezaji huyo wa Barcelona aliokota ndizi aliyokuwa ametupiwa na kuila kabla ya kuitupa na kuendelea na mchezo. Rais wa Brazil amuunga mkono Alves Klabu ya Villarreal inasema kuwa imempiga marufuku mwanaume ambaye alitupa ndizi hiyo uwanjani na kuwa hatohudhuria mechi zote za nyumbani za klabu hiyo maishani. Mamia ya watu na wachezaji maarufu duniani wameonyesha upendo wao kwa mchezaji huyo kwa kuweka picha zao kwenye mitandao wa kijamii wakila ndizi. Mchezaji wa Manchester City Sergio Aguero alipachika picha akila ndizi sawa na nyota ya soka y...

Arsenal 3-0 Newcastle

Image
Arsenal ya Uingereza ilijiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu kwa mchuano wa ligi ya mabingwa mwakani baada ya kuinyuka Newcastle mabao matatu kwa nunge katika mechi ya katikati ya juma iliyochezwakatika uwanja wao wa nyumbani wa Emirati. Laurent Koscielny ndiye aliweka niya ya 'the Gunners' bayana alipofunga mkwaju wa Santi Cazorla kunako dakika ya 26 ya kipindi cha kwanza . Mesut Ozil naye akaongezea la pili kabla ya kukamilika kipindi cha kwanza .Ushindi huo umeiacha Arsenal na jumla ya alama 73 nne zaidi ya wapinzani wao wa karibu Everton wenye alama 69. Hata hivyo ni Olivier Giroud ndiye aliyemhakikishia kocha Arsene Wenger alama tatu muhimu alipohitisha kichapo hicho kwa bao la tatu kunako dakika ya 66 ya mechi hiyo. Aidha ilikuwa ni kichapo cha 6 mfululizo kwa timu ya Newcastle na kocha Alan Pardew . Hata hivyo mbivu na mbichi itabainika Manchester City itakapokwaruzana na Everton jumamosi ijayo. Timu nne za kwanza ndizo zinazoshiriki mchuano huo wenye kitita...

Suarez ndiye mchezaji bora katika EPL

Image
Mshambulizi wa Liiverpool Luis Suarez, ametajwa kuwa mchezaji mwenye tajriba na maarifa ya hali ya juu mwaka huu. Suarez mwenye umri wa miaka 27 alisafiri kuelekea katika sherehe hizo baada ya wao kushindwa na timu ya Chelsea. Akizungumuza katika sherehe hiyo Suarez alisema kuwa. Suarez kufikia sasa amefunga mabao 30 na ndiye anayeongoza matumaini Liverpool kukatisha ukame wa miaka 24 tangu watwae taji la ligi kuu ya Uingereza. Suarez atakumbukwa zaidi kwa kisa kilichogonga vichwa vya habari duniani baada ya kumngata mchezaji wa Chelsea Branislav Ivanovic. Suarez alipigwa marufuku ya mechi Kumi baada ya kupatikana na hatia . Wengine walioteuliwa ni Eden Hazzard wa Chelsea aliyetajwa kama mchezaji mchanga wa mwaka huu. Daniel Sturridge na naodha wa Liverpool Steven Gerrard walijiunga na Suarez kutokana ushirikiano wao iliyopelekea Liverpool kutajwa kama klabu bora ya mwaka huu. Waliokuwemo ni pamoja na Kipa wa Chelsea Peter Czech na mlinzi Gary Cahil. Hata hivyo msu...

Droo ya CAF 2015

Image
Droo ya Kufuzu kwa kombe la mataifa Afrika mwakani{ Afcon} imefanyika huko cairo Misri huku timu zote za kanda ya Afrika Mashariki zikiratibiwa kucheza katika mechi za mchujo kabla ya kushirikimechi za kufuzu . Kenya itachuana dhidi ya Visiwa vya Comoro ,Tanzania ipambane na Zimbabwe, Uganda imeratibiwa kutoana kijasho dhidi ya Madagascar nayo Rwanda ikivaana na Libya. Raundi ya Kwanza Liberia v Lesotho Kenya v Comoros Islands Madagascar v Uganda Mauritania v Equatorial Guinea Namibia v Congo Libya v Rwanda Burundi v Botswana Central African Republic v Guinea Bissau Swaziland v Sierra Leone Gambia v Seychelles Sao Tome e Principe v Benin Malawi v Chad Tanzania v Zimbabwe Mozambique v South Sudan Baada ya kushiriki mkondo wa kwanza wa maondoano mataifa hayo tena yatalazimika kuchuana miongoni mwao ilikufuzu kwa awamu ya pili .Burundi kwa upande wake itachuana dhidi ya Botswana, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ikiratibiwa kuvaana na Namibia. Mshindi wa ...

Chelsea yaiadhibu Liverpool 2-0

Image
Chelsea vijana wa darajani Stanford, jijini London, wamewanyamazisha vinara wa ligi kuu ya England, Liverpool baada ya kuwachakaza mabao 2-0 katika uwanja wao wa Anfield. Liverpool ikiwa imeuanza mchezo huo kwa kasi na kwa dhamira ya kupata ushindi ilishuhudia jahazi lake likitota katika dakika ya 45 ya kipindi cha kwanza. Demba Ba mfungaji wa bao la kwanza la Chelsea                                                                                                                                                                                  ...

G7 kuiwekea Urusi vikwazo zaidi

Image
Viongozi wa nchi zenye uwezo mkubwa duniani G7 wamekubaliana kuiwekea vikwazo zaidi Urusi, wanayosema inaendelea kuchochea ghasia mashariki mwa Ukraine. katika taarifa yao, viongozi hao walionyesha wasiwasi wao kuhusu jitihada za wanaharakati wanaounga mkono Urusi kuendelea kuyumbisha mashariki mwa Ukraine. Hatahivyo viongozi hao wameipongeza Ukraine kwa kujizuia katika kukabiliana na makundi ya wanamgambo yaliojihami.Urusi ,wamesema haijachukua hatua zozote kutekeleza makubaliano ya mjini Geneva mbali na kuwaamrisha wanamgambo hao kuondoka katika majengo ya serikali wanayodhibiti. Wakati huohuo, wanamgambo wanaounga mkono Urusi mashariki mwa mji wa Ukraine wa Slavianski wamelitekanyara kundi moja la wachunguzi 13 wa kimataifa pamoja na wale wa Ukraine ambao walikuwa wanazuru eneo hilo wakiwa miongoni mwa ujumbe unaoshirikishwa na shirika la usalama la muungano wa Ulaya. Kundi hilo linashirikisha wachunguzi wa kijeshi wa Ujerumani pamoja na wawakilishi wa Denmark,Poland,Sweden ...

Obama awasili Korea Kusini kushauriana

Image
Rais Obama amewasili Korea Kusini huku hofu ikizagaa kwamba Korea Kaskazini huenda inajiandaa kufanya jaribio la nne ya zana zake za nukyla. Inatarajiwa kwamba shughuli mpya katika kinu cha nuklya mjini Pyongyang zitatawala mazungumzo kati ya bwana Obama na rais wa Korea Kusini Park Geun-hye. Viongozi hao wawili wanarajiwa kuangazia zaidi jukumu la Uchina katika kuithibiti Korea Kaskazini, jambo ambalo Bwana Obama ametaja kuwa lenye  umuhimu mkubwa. Rais wa Marekani Barack Obama amewasili Korea Kusini katika sehemu yake ya pili ya ziara katika Bara la Asia. Anatarajiwa kukutana na Rais Park baadaye leo na kuwatembelea wanajeshi wa Marekani walioko nchini humo. Ziara yake inafanywa wakati ambapo kuna hofu kuwa Korea Kaskazini huenda ikafanya jaribio la nne la Kinukilia. Korea Kaskazini inatarajiwa kujadiliwa na viongozi hao wawili na tayari kuna ripoti kuwa maandalizi ya kufanya jaribio la Kinukilia yanayoendelea kufanywa Korea Kaskazini yatahakikisha kuwa taifa hilo ji...

Ryan Giggs azungumzia Man U

Image
Ryan Giggs amefanya mkutano wake wa kwanza na waandishi wa habari kama meneja wa muda wa timu ya soka ya Manchester United kufuatia kufutwa kazi kwa David Moyes mapema wiki hii . Ameelezea siku chache zilizopita zimekuwa kama fujo tupu kwa klabu hiyo na akaahidi kujaribu kurejesha tabasamu kwenye nyuso za mashabiki . Hii ni kufuatia kufutwa kazi kwa meneja wa klabu hiyo David Moyes kutokana na matokeo mabaya ya klabu hiyo katika ligi ya Premier. Alianza kwa kumshukuru Meneja wa zamani Moyes kwa kumpatia fursa ya kwanza kufanya kazi kama kocha.

Ukawa nusura ‘wamchenjie’ Mbowe

Image
Dodoma. Wajumbe wa Mkutano wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), juzi nusura wamgeuzie kibao mwenyekiti wao, Freeman Mbowe baada ya kuchelewa kufika kwenye mkutano ulioandaliwa ikiwa ni siku moja baada ya kususia kikao cha Bunge la Katiba. Ukawa walikutana kwenye Ukumbi wa African Dream kwa ajili ya kujipanga baada ya kususia mkutano wa Bunge. Mkutano huo ulioanza saa 4:18 ukiongozwa na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba baadaye wajumbe walianza kuhoji walipo viongozi wao, Freeman Mbowe na James Mbatia. Mmoja wa wajumbe wa mkutano huo, Profesa Abdallah Safari alisimama na kuhoji walipo viongozi hao hatua iliyoanza minong’ono miongoni mwa wajumbe wakiwa na hisia kwamba huenda wamewageuka na kwenda kwenye Kikao cha Kamati ya Uongozi. “Tujue kabisa kama wametugeuka...Tumeshakubaliana hakuna mtu kwenda kwenye Mkutano wa Kamati ya Uongozi, sasa kama amekwenda tujue,” ilisikika sauti ya mmoja wa wajumbe. Kuona hivyo, ilibidi Profesa Lipumba aanze kuwapigia sim...

Mbowe: Hakuna aliyemtusi Mwalimu Nyerere, wala anayetaka kuvunja Muungano

Mwenyekiti wa Umoja wa Katiba ya Watanzania (Ukawa), Freeman Mbowe, amesema uamuzi wao wa kutoka nje ya Ukumbi wa Bunge ni sahihi kwa kuwa ni njia ambayo imeonekana kwao kuwa inafaa kudai haki ya Watanzania wote. Mbowe ambaye pia ni kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, alisema hayo muda mfupi baada ya kumalizika kwa mkutano wa ndani wa Ukawa. Mkutano huo pamoja na mambo mengine ulijadili mikakati mbalimbali inayohusu umoja huo ambao sasa wanapeleka masuala yao kuhusu mchakato wa Katiba Mpya kwa wananchi. Ukawa pamoja na baadhi ya wajumbe wa Bunge la Katiba kutoka kundi la 201, walitoka nje ya Ukumbi wa Bunge mjini wakidai kutoridhishwa na mwenendo wa Bunge hilo lenye lengo la kutengeneza Katiba Mpya. “Kuendelea kushiriki mchakato huu, ni kuubariki na kuupa uhalali udhalimu unaoendelea ndani ya Bunge Maalumu, hatuwezi kushiriki mjadala wenye matusi, kejeli, dharau na unaopotosha umma, kwa kupindisha kauli zilizowahi kutolewa na viongozi wetu,’ anaeleza Mbowe. ...

REAL MADRID KUILAZA FC BARCELONA

Image
Bale asherekea bao la ushindi dhidi ya Barcelona  ni baada ya mshambuliaji bale kupachika bao dakika za mwisho,kitendo kilichopelekea madrid kuutwa ubingwa wa copa del rey jijini hispania............ Barcelona ambayo imekuwa ikishuhudia msururu wa matokeo yasiyo ya kuridhisha katika siku za hivi punde inafunga orodha ya tatu bora ikiwa na alama 78. Madrid sasa inamuda wa kutoka kujiandaa kwa mechi ya nusu fainali ya kombe la mabingwa barani Ulaya dhidi ya mabingwa watetezi Bayern Munich ya Ujerumani. Mechi nyingine ya nusu fainali ya kombe la mabingwa barani Ulaya itakuwa kati ya Chelsea ya Uingereza dhidi ya Atletico Madrid. Nusu fainali hizo zitachezwa juma lijalo.